Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema kuwa wanafanya juhudi kubwa kuhakikisha wanawaondoa wanajeshi wao waliojeruhiwa katika jimbo la Mariupol.
Zelensky ametoa kauli hiyo katika matangazo ya kila wiki ambayo amekuwa akiyatoa tangu taifa lake lilipovamiwa na Urusi.
Itakumbukwa kwamba Urusi inataka sana kuchukua udhibiti wa mji wa Mariupol, ambao wamekuwa wakiupiga kwa makombora kwa miezi sasa.
Jeshi limetoa wito wa kuomba msaada baada ya wanajeshi wengi kujeruhiwa.
Katika hotuba hiyo, Rais Zelensky alisema kuwa wameanza mazungumzo ya kuangalia iwapo vikosi vya Urusi vitaruhusu kuwaondoa majeruhi amesema pia yalikuwa ni mazungumzo magumu mno.