Star Tv

Panya maarufu na shujaa wa Tanzania aliyetumika kutafuta na kutegua mabomu ya ardhini na vilipuzi kwa jina la Magawa amefariki dunia mwishoni mwa wiki hii.

Kupitia taarifa iliyotolewa katika ukurasa wa instagram wa shirika la Apopo limesema Magawa alikuwa na afya njema wiki iliyopita lakini afya yake ilianza kudhoofika mwishoni mwa wiki na kuaga dunia akiwa na umri wa miaka minane.

Panya huyo alisifika sana kwa kusaidia kugunduliwa kwa Zaidi ya mabomu 100 ya kutegwa ardhini nchini Cambodia.

"Mchango wake unaruhusu jamii nchini Cambodia kuishi, kufanya kazi na kucheza; bila hofu ya kupoteza maisha au kiungo. Mnamo Septemba 2020, alikabidhiwa rasmi Medali ya Dhahabu ya PDSA - tuzo ya juu zaidi ya ushujaa ambayo mnyama anaweza kupokea. Mwaka jana wakati Magawa alipostaafu, HeroRAT Ronin alichukua kijiti kama panya mpya wa kuasili"- Imebainishwa katika sehemu ya taarifa iliyotangaza kifo cha panya huyo.

#ChanzoBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.