Star Tv

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango leo tarehe 18 Novemba 2021 ametembelea Bandari ya nchi ya Singapore na kujionea namna inavyofanya kazi.

Katika ziara hiyo Makamu wa Rais ameshuhudia teknolojia mbalimbali zinazotumika katika kufanya kazi katika bandari hiyo ikiwemo upakuaji na upakiaji makasha na mizigo, ukaguzi wa mizigo pamoja na ufuatiliaji makasha wakati wote yanapokuwa safarini.

Akitoa maelezo namna bandari hiyo ilivyopiga hatua kubwa katika kipindi cha muda mfupi Makamu wa Rais wa Mamlaka ya Bandari ya Singapore anayeshugulikia masuala ya biashara bwana Ong Seow Leong amesema bandari hiyo imewekeza katika mafunzo pamoja na ubunifu uliopelekea kuongezeka kwa teknolojia inayotumika hivi sasa katika kutoa huduma ikiwemo kuweza kufanikiwa kushusha na kupakia makasha laki moja ndani ya siku moja.

Amesema bandari ya Singapore imekuwa na mtandao na bandari zingine duniani hivyo kuongeza ufanisi wa ufanyaji kazi wa bandari hiyo.

Aidha ameongeza kwamba Bandari ya Singapore imekuwa ikiweka mkazo katika kutafuta masoko pamoja na kufanya tafiti zinazoweza kuongeza watumiaji wa bandari hiyo.

Katika hatua nyingine Bwana Leong ameeleza kuwa ni lazima kuwepo na mipango ya muda mrefu katika uendeshaji wa bandari na tayari nchi ya Singapore inaendelea na ujenzi wa bandari mpya na ya kisasa ambayo kwa miaka ijayo itaweza kutoa huduma kwa ufanisi zaidi.

Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango amesema Tanzania itashirikiana na Uongozi wa Bandari ya Singapore katika kutoa mafunzo kwa watumishi wa bandari za Tanzania pamoja na kupeleka watalaamu wa bandari kutoka Singapore kwenda Tanzania ili kushirikiana katika kufanya maboresho ya haraka hasa katika bandari ya Dar es salaam.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.