Star Tv

Rais wa mwisho mzungu wa Afrika Kusini FW de Klerk, aliyefariki akiwa na umri wa miaka 85 wiki iliyopita, atazikwa katika sherehe ya faragha siku ya Jumapili, kulingana na wakfu wake.

Taarifa iliyotolewa na Familia yake ilibainisha kuwa, “Wakfu wa FW de Klerk unawatangazia kuwa kuchomwa kwa FW de Klerk’ na mazishi yake itafanyika Jumapili Novemba, 2021,”.

“Itakua shere ya faragha kwa familia na haitakua wazi kwa vyombo vya habari,”- Wakfu huo uliongeza na hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa.

De Klerk aliingia madarakani mwaka 1989 chini ya utawala wa ubaguzi wa rangi, mfumo ambao ulihalalisha ubaguzi wa rangi, lakini baadaye akawa mtu muhimu katika kipindi cha mpito kuelekea demokrasia.

Mwaka 1993, alipata Tuzo ya Amani ya Nobel na rais wa zamani Nelson Mandela kwa kusaidia kujadili kukomesha ubaguzi wa rangi.

Alifariki Alhamisi baada ya kupatikana na saratani mapema mwaka huu.

#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.