Raia kadhaa wa mataifa ya kigeni pamoja na wengine wa nchini Madagascar wanashikiliwa na mamlaka nchini humo kwa tuhuma za jaribio la mauaji ya Rais Andry Rajoelina.
Mwanasheria mkuu wa serikali nchini humo amesema kwenye taarifa yake kwamba raia wawili wa Ufaransa ni miongoni mwa waliokamatwa.
Watu hao kadhaa wamekamatwa kwa kutaka kumuua Rais wa Taifa hilo la Kisiwa ikiwa ni sehemu ya uchunguzi unaohusiana na kudhoofisha hali ya usalama wa taifa hii pia ikiwa ni kulingana na duru za kidiplomasia.
Rajoelina alikula kiapo cha Urais mwaka 2019 baada ya uchaguzi mgumu ambao ulipingwa kwenye mahakama ya kikatiba kutoka kwa wapinzani wake.
#ChanzoBBCSwahili