Star Tv

Wanaume wawili wamejaribu kumdunga kisu Rais wa mpito wa Mali Assimi Goïta katika msikiti uliopo katika mji mkuu, Bamako.

KanaliGoïta allikuwa akihudhuria ibada ya siku ya Eid ul-Adha katika msikiti wa Grand Mosque.

Mafisa wanasema washambuliaji, ambao kwa mujibu wa Shirika la habari la AFP walikuwa ni wawili, wamekamatwa na rais ameondolewa kwenye msikiti huo kwa usalama wake.

Haijafahamika iwapo Kanali Goïta, ambaye aliongozajeshi kuchukua mamlaka mwezi Agosti, alijeruhiwa.

Waziri wa masuala ya kidini Mamadou Kone aliliambia shirika la AFP kwamba mwanaume ali "jaribu kumuua rais wa kisu".

Mkurugenzi wa msikiti aliliambia shirika la habari kwamba mtu alimlenga waziri lakini alimjeruhi mtu mwingine.

Kabla ya mapinduzi ya mwezi Agosti nchi hiyo ilikuwa inakabiliwa na maadamano juu ya ufisadi na waasi wa Kiislam walikuwa wameyateka maeneo mengi ya nchi.

#ChanzoBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.