Star Tv

Mamlaka ya mapato nchini Kenya (KRA) inatarajiwa kuzifungia jumla ya nambari ya siri 66,269 za kulipa kodi ambazo hazitumiki kufikia Alhamisi wiki hii, ripoti za vyombo vya habari nchi humo zimesema.

Wamiliki wa nambari hizo za siri za kulipa kodi ambao ni pamoja na watu binafsi na mashirika ya biashara huenda wakafutiwa usajili malipo ya ushuru wa bidhaa.

Walipa kodi watakaoathiriwa watazuiwa kutoza ada ya ushuru wa bidhaa katika biashara zao na huenda wakakabiliwa na vikwazo vingine vya utozaji ushuru.

Hatua kama hiyo pia itachukuliwa dhidi ya watu ambao hawajakuwa wakijaza fomu ya kuthibitisha wanalipa kodi kwa mujibu wa sheria.

“Kufutiwa kwa jukumu la kulipa ushuru wa bidhaa ni mpango unaoendelea, utawaathiri walipa kodi ambao hawatajaza fomu ya kila mwezi ya kuthibitisha wamelipa ushuru wa bidhaa au wale ambao hawaoneshi jinsi walivyolipa ushuru huo kila mwezi miongoni mwa mambo mengine,”-KRA ilisema katika taarifa yake kwa umma.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.