Star Tv

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Gutterres amesema maeneo kadhaa katika jimbo la Tigray Kaskazini mwa Ethiopia yanakabiliwa na tisho la baa la njaa.

Gutterres ameonya, kwa kusema kuwa hali inaendelea kuwa mbaya zaidi endapo ufadhili hautaongezwa na njia za kufikia walioathiriwa haitaimarishwa.

''Hatua tunazochukua sasa zinaweza kuwaokoa watu wengi walio katika hatari ya kuangamia kutokana na ukosefu wa chakula"- alisema Gutterres.

Wakazi wa Magharibi mwa Tigray wameiambia BBC kwamba hawana chakula na kwamba wanakabiliwa na baa la njaa.

Watu wa wilaya ya Qafta Humera waliofikiwa kwa nji aya simu wamesema majambazi wamevamia mashamba yao na kuchukua mifugo yao.

Mark Lowcock ameiambia BBC kwamba mamia ya watu tayari wanakabiliwa na njaa katika eneo la Tigray kufuatia miezi kadhaa ya mapigano.

Mamlaka nchini Ethiopia inasisitiza kwamba hali ya utulivu imerejeshawa katika eneo hilo na njia za kuwafikia wakazi kufunguliwa.

Lakini UN inasema maelfu ya watu sasa wanaelekea kukabiliwa na baa la njaa kama lile lililoshuhudiwa mwaka 1984.

Mzozo ulizuka Tigray mwezi Novemba baada ya serikali ya Ethiopia kuanzisha oparesheni ya kijeshi ya kuondoa mamlakani chama tawala cha zamani TPLF, baada ya wapiganaji wake kuteka kambi za jeshi la muungano.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.