Star Tv

Wizara ya mambo ya ndani ya Iraq imesema watu 82 wamekufa huku wengine 110 wakijeruhiwa katika mkasa mkubwa wa moto katika vyumba vya wagonjwa mahututi katika hospitali moja mjini Baghdad inayowahudumia wagonjwa wa virusi vya corona.

Mamlaka ya hospitali hiyo imelaumiwa kwa uzembe kufuatia moto huo unaosemekana ulitokea baada ya mitungi ya gesi ya hewa ya Oksijeni kuripuka katika hospitali ya Ibn al Khatib.

Waziri Mkuu wa Iraq Mustafa al-Kadhimi aliwafuta kazi maafisa kadhaa wa hospitali hiyo saa chache baada ya mkasa wa moto.

Wizara ya afya nchini humo imesema watu 200 waliokolewa lakini hadi sasa bado baadhi ya jamaa za wagonjwa wangali wanaitafuta miili ya wapendwa wao.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.