Star Tv

Wasafiri wanaoelekea Ireland kutoka Kenya watalazimika kujitenga kwa wiki mbili baada ya kuwasili katika nchi hiyo ya bara Ulaya.

Siku ya Jumamosi, Dublin iliongeza Kenya na nchi nyingine kadhaa kwenye toleo lake la orodha ya nchi zilizowekea vikwazo vya usafiri kwa ajili ya Covid-19, ambazo wasafiri wake lazima wangeweka mapema hoteli watakazotumia kama karantini.

Maafisa walisema agizo hilo ambalo linaanza kutumika mnamo Aprili 15 linalenga kuzuia kuenea kwa virusi vya Corona.

Nchi nyingine tano ziliongezwa kwenye orodha huku kukiwa na wasiwasi juu ya aina mpya za Covid-19

Nchi nyingine ni pamoja na Ubelgiji, Ufaransa, Italia, Luxemburg, Marekani , Canada, Bangladesh, Pakistan, Uturuki, Armenia, Bermuda, Bosnia na Herzegovina, CuraƧao, Maldives na Ukraine.

Wasafiri kutoka Kenya watahitajika, kuanzia saa 4 asubuhi Alhamisi hii kujiandikisha katika hoteli zilizotengwa za karantini kwa gharama zao wanapowasili Ireland.

"Mipangilio hii inatumika kwa abiria yeyote ambaye amekuwa katika yoyote ya nchi hizi katika siku 14 zilizopita, hata ikiwa anapitia mojawapo ya nchi hizi na hata ikiwa amebaki barabarani,"- Sehemu ya taarifa kutoka kwa tovuti ya ubalozi wa Ireland imesema.

Chanzo:BBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.