Star Tv

Maafisa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamesema zaidi ya watu 60 wamezama baada ya mashua kupinduka na kuzama katika mto Congo.

Mamlaka za nchini humo zimeeleza kuwa watu 300 wameokolewa lakini inakisiwa kuwa watu wengine 200 hawajulikani walipo baada ya ajali hiyo.

Wakazi wanasema boti iligonga mwamba mashariki mwa mji mkuu Kinshasa, wakati walipokuwa wakisafiri usiku.

Safari za majini nyakati za usiku zimepigwa marufuku nchini humo.

Waziri wa masuala ya kibinadamu, Steve Mbikayi, ametaka wale wamiliki wa boti kushtakiwa.

"Chombo kilichojaa kupita kiasi, kilichokuwa na abiria zaidi ya 700 kilipinduka Mai-Ndombe! Miili 60 tayari imepatikana na watu 300 wamenusurika Tunazipa pole familia zilizofiwa na tunataka hatua zichukuliwe dhidi ya wale wote wanaohusika na sekta ya uchukuzi"- aliandika Waziri huyo kwenye mtandao wa Twitter.

Aidha, imeeelezwa kuwa kuna barabara chache nchini DRC na shughuli nyingi za usafiishaji wa mizigo na abiria ambao hufanywa kwa njia ya mto.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.