Star Tv

Desemba 1, 1990, Idriss Déby alichukua hatamu ya uongozi wa nchi ya Chad kufuatia mapinduzi ya kijeshi yaliyomuondoa, Hissène Habré.

Ni miaka miaka 30 tangu Idriss Déby, achukue madaraka kabla ya kupewa cheo cha marshal mwanzoni mwa mwaka huu.

Miaka 30 iliyopita, Desemba 1, 1990, akiwa kiongozi wa kundi la wapiganaji la Wokovu wa Uzalendo, MPS, Idriss Déby aliuteka mji wa Ndjamena, mji mkuu wa Chad alioukimbia mtangulizi wake Hissène Habré ambaye vikosi vyake vilishindwa kuhimili mashambilizi ya vikosi vya MPS.

Desemba 4 Idriss Débyaliteuliwa kuwa rais wa Baraza la taifa, wakati Hissène Habré akikimbilia Senegal.

Miezi ishirini mapema, mnamo Aprili 1, 1989, Idriss Déby na washirika wake wachache ambao walitafautiana na kiongozi wao Hissène Habré walijaribu kufanya mapinduzi.

Watu hao walioshirikiana na Idriss Déby, ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani Mahamat Brahim Itno, na Hassan Djamouss, Amiri Jeshi Mkuu wa jeshi la Chad.

Lakini mpango wao wa mapinduzi ulitibuliwa, washirika wake watatu na askari kadhaa walijaribu kuondoka Chad kuelekea Sudan.

Kutoka Sudan, Kanali Idriss Déby alifanikiwa kushirikiana na makundi mbalimbali ya upinzani dhidi ya Hissène Habré na mnamo Machi 11, 1990 aliunda kundi la wapiganaji la MPS katika eneo la Bamina nchini Sudan.

Rais wa Chad Hissène Habré wakati huo alikataa kutii agizo la mwenzake wa Ufaransa François Mitterrand, ambaye aliomba katika hotuba yake katika mkutano wa Ufaransa na Afrika huko La Baule mnamo 1989 kwamba serikali madarakani barani Afrika zinatakiwa kuanzisha mfumo wa vyama vingi na demokrasia ikiwa zinataka kuendelea kuungwa mkono na Ufaransa.

Habré, ambaye aliamua kupinga mamlaka ya zamani ya kikoloni, alipingana na kauli hiyo kwa kuandaa uchaguzi wake kwa muhula wa miaka saba mwezi Desemba 1989.

Uchaguzi wa wabunge uliruhusu kuanzishwa kwa Bunge ambalo halikuridhishwa na mfumo wake wa kidemokrasia.

Kulingana na baadhi ya wachambuzi, nia ya rais wa Chad kutumia mafuta ya Chad kwa gharama zote akiungwa mkono na Marekani ambapo alikuwa mmoja wa washirika wakuu katika vita dhidi ya Muammar Gaddafi wa Libya, ni mpoja ya sababu ya kuanguka kwa utawala wake.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.