Star Tv

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dkt.Bashiru Ally ameongoza mamia ya waombolezaji kuaga miili 10 ya wanafunzi waliofariki kwa kuungua na moto.

Ajali hiyo iliyotokana na moto ambao chanzo chake hakikujulikana mpaka sasa, uliteketeza bweni la watoto wa kiume katika shule ya msingi Byamungu Islamic iliyoko wilayani Kyerwa Mkoani Kagera na kupelekea watoto 10 kupoteza maisha papohapo.

Wanafunzi hao walifarika usiku wa kuamkia tarehe 14 Septemba, 2020, huku wanafunzi saba wakiwa wamejeruhiwa na mpaka sasa watano kati yao wanaendelea na matibabu katika hospitali ya Rufaa ya Bugando iliyopo jijini Mwanza.

Jumla ya wanafunzi waliokuwepo kwenye bweni hilo wakati ajali hiyo ya moto inatokea ni 74.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.