Star Tv

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli ametangaza siku 07 za maombolezo ya kitaifa kuanzia Ijumaa ya leo Julai 24, kufuatia kifo cha rais mstaafu wa awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa kilichotokea Dar es Salaam.

Rais amesema kuwa katika kipindi chote bendera zitapepea nusu mlingoti.

Aidha Rais Magufuli amewaomba Watanzania wote kuendelea kuwa watulivu, wastahimilivu na wamoja katika kipindi hiki kigumu cha majonzi cha kuondokewa na mpendwa wao rais Mstaafu Mkapa.

Rais huyo mstaafu wa serikali ya awamu ya tatu amefariki akiwa na miaka 81.

Rais John Pombe Magufuli alitangaza usiku wa kuamkia leo Ijumaa kupitia runinga ya taifa taarifa za kufariki dunia kwa Mzee Mkapa katika hospitali moja jijini Dar es Salaam alipokuwa amelazwa kwa matibabu.

''Mzee Benjamin William Mkapa Rais wa awamu ya tatu amefariki. Amefariki kwenye hospitali mjini Dar es Salaam ambako alikuwa amelazwa. Niwaombe watanzania tulipokee hili. Taifa limepata msiba mkubwa. Tuendelee kumuombea Mzee wetu Rais Benjamin William Mkapa ambaye ametangulia mbele ya haki," alitangaza rais Magufuli.

Taarifa hiyo hata hivyo haikuweka wazi Rais Mkapa alikuwa akisumbuliwa na maradhi gani.

Katika ukurasa rasmi wa Rais Magufuli wa mtandao wa Twitter rais Magufuli amemuomboleza Mkapa na kusema atamkumbuka "kwa mapenzi yake makubwa kwa Taifa, ucha Mungu, uchapakazi na utendaji wake katika kujenga uchumi."

RaisĀ Mkapa alizaliwa Novemba 1938, Mkoani Mtwara Kusini mwa Tanzania, na aliliongoza taifa hili la Tanzania kwa mihula miwili toka mwaka 1995 mpaka 2005.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.