Star Tv

Mkuu wa Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Rosemary Staki amesema uwepo wa Reli wilayani humo utasaidia kukuza uchumi kwa wananchi pamoja na kusafirisha madini ya Gypsum.

Taarifa na Angela Mathayo

Mkuu huyo wa Wilaya ya Same ametoa kauli hiyo wakati Shirika la Reli Tanzania TRC limewasafirisha wananchi wa Wilaya ya Same zaidi ya 400 kwa kutumia usafiri wa Treni , kutoka Stesheni ya Moshi kuelekea Steseheni ya Same Mkoani Kilimanjaro,

Wananchi hao wamesafari umbali wa zaidi ya kilomita 100 wakitumia usafiri wa mabasi kutoka Wilayani Same  hadi Moshi Mjini, kwa lengo la kupanda Treni ya Abiria ya Deluxe na kurejea tena Same ikiwa ni sehemu ya kutambua na kupongeza juhudi za Rais Magufuli za kurejesha usafiri huu ambao ulisimama kwa zaidi ya miaka 25.

Usafiri huo wa treni umetajwa kuwa  kimbilio la wengi, ambapo hadi sasa zaidi ya abiria elfu kumi wamesafirishwa na usafiei huo tangu kurejea baada ya miaka 26.

Katika safari hiyo watu mbalimbali wameshiriki wakiwemo wanafunzi ,kutoka shule mbalimbali za Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro.

                                                                                   Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.