Star Tv

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Angellah Kairuki amesema Serikali imetoa Shilingi bilioni 13.88 kwa ajili ya kuboresha huduma za afya katika Mkoa wa Kigoma.

Kairuki ameyabainisha hayo katika ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzungumza na wananchi wa Mkoa wa Kigoma kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika.

Amesema kati ya fedha hizo zilizotolewa kwa mwaka 2021/22, Sh bilioni 6.6 zimetumika katika ujenzi na ukamilishaji wa vituo vya afya 15 na bilioni 1.2 zimeelekezwa kwenye ukamilishaji wa ujenzi wa Zahanati 24 katika Mkoa wa Kigoma.

Aidha pia amebainisha kuwa Sh bilioni 3.5 zilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali katika halmashauri 6 za Buhigwe, Kakonko, Kasulu DC, Kigoma DC, Kigoma MC na Uvinza DC.

Kuhusu miundombinu ya barabara, Kairuki amesema, Serikali imetoa Sh bilioni 21.7 kwa ajili ya kuimarisha barabara na imepanga kuitumia bilioni 34.1 kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Uboreshaji Miji (TACTIC) ambao umelenga kuboresha miundombinu katika Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.