Rais wa Tanzania Samia Suluhi Hassan ameipongeza klabu ya Simba kwa kufanikiwa kufuzu hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya timu ya Primeiro de Agosto ya Angola.
Rais Samia ametoa pongezi hizo kupitia ukurasa wake wa twitter pamoja na kuwatakia kila la heri katika michuano inayofuata.
Mchezo huo uliochezwa katika uwanja wa taifa na umeiibua timu ya simba kuwa mshindi kwa bao lililofungwa na Moses Phiri.
Aidha katika mchezo wa kwanza Angola, Simba iliibuka na ushindi wa mabao 3-1, na sasa imefuzu kwa jumla ya mabao 4-1.