Star Tv

Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania, (TANAPA), limefungua fursa kwa wawekezaji wa ndani ya Tanzania kutembelea vivutio vinavyopatikana katika hifadhi za kanda ya Magharibi kkwa lengo la kuwekeza katika huduma mbalimbali. Hii inatokana na idadi ndogo ya watalii wa ndani na nje wanaotembelea hifadhi za ukanda huo.

Ofisi za kanda ya Magharibi ambazo zinajumuisha hifadhi 10 ambazo ni, Serengeti, Kisiwa cha Saanane, Burigi- Chato, Kisiwa cha Rubondo, Mto Ugalla, Kigosi, Ibanda-Kyerwa, Rumanyika Karagwe, Gombe na Milima ya Mahale.

Ziara hii imeongozwa na Kamishna msaidizi Beatrice Kessy- msimamizi kitengo cha maendeleo ya Biashara, Utalii na masoko katika hifadhi za taifa kutoka makao makuu ya TANAPA. Ambapo wawekezaji hawa wamepata fursa za kutembelea hifadhi hizi na kujionea vivutio vilivyopo hifadhini. wakianzia hifadhi za Gombe na milima ya Mahale hifadhi maarufu kwa kuwa na sokwe wakubwa. Ziara hii ikiwa ya siku 10 wawekezaji hoa watatembelea hifadhi 7 kati ya kumi ambazo ni, Burigi- Chato, Kisiwa cha Rubondo, Mto Ugalla, Ibanda-Kyerwa, Rumanyika Karagwe, Gombe na Milima ya Mahale.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.