Star Tv

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kuendeleza zao la zabibu ili kuhakikisha linaleta tija kwa wakulima.

Waziri Mkuu amebainisha hayo wakati alipotembelea Kituo cha Utafiti wa Kilimo Tanzania katika eneo la uzalishaji miche ya zabibu, mashamba na viwanda vya zabibu, Dodoma.

“Serikali imeanzisha kampeni ya kuhamasisha kilimo cha zao la zabibu, tunataka kumsaidia mkulima kuanzia maandalizi ya shamba, upatikanaji wa pembejeo hadi hatua ya mauzo.”

Waziri Majaliwa ametembelea kituo hicho cha utafiti kuona uwezo wake wa kuzalisha mbegu, pia ametembelea mashamba ya wakulima katika eneo la Msalato na Hombolo ili kuhamasisha kilimo hicho.

Pia, Waziri Mkuu ametembelea kiwanda vya kuchakata zabibu kikiwemo kiwanda kidogo cha mkulima mdogo wa zabibu Bw. Phortunatus Kenyunko kilichopo eneo la Msalato, jijini Dodoma.

Mbali na kutembelea kiwanda hicho kidogo, pia Waziri Mkuu ametembelea kiwanda kikubwa cha kutengeneza mvinyo wa zabibu cha Cetawico kiilichopo Homboro, jijini Dodoma.

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwahakikishia wakulima wa zabibu kwamba Serikali imedhamiria kuboresha kilimo cha zao hilo kwa sababu kilimo ni mkombozi kwa Watanzania.

Amesema kampeni hiyo itanzia mkoa wa Dodoma kwa kuwa imegundua kwamba zabibu ni fursa ya kiuchumi nchini na ardhi yote ya wilaya za mkoa wa Dodoma inakubali kilimo hicho.

Katika kuhakikisha kilimo hicho kinapata mafanikio, Waziri Mkuu amezitaka taasisi za kifedha ikiwemo Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ibadilike na kutoa mikopo kwa wakati.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.