Star Tv

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 31 Mei, 2021 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Miradi wa taasisi ya The Susan Thompson Buffet Foundation Bi. Senait Fisseha ambayo inajihusisha na masuala ya afya ya wanawake.

Bi. Senait Fisseha amemueleza Mhe. Rais Samia kuwa taasisi hiyo ambayo imekuwepo hapa nchini kwa zaidi ya miaka 10 imetumia dola za Marekani takribani Milioni 90 (sawa na shilingi Bilioni 206) kufadhili miradi ya inayoshughulikia changamoto mbalimbali zinazohusiana na afya ya uzazi kwa wanawake na wasichana.

Amebainisha kuwa miradi hiyo imesaidia kukabiliana na vifo vinavyohusiana na ujauzito kwa kuwawezesha wanawake kupanga wakati gani wa kupata ujauzito, wakati gani wa kujifungua, kuepuka ujauzito katika umri mdogo na kujifungua salama.

Bi. Senait Fisseha ameshukuru kupata nafasi ya kuzungumza na Mhe. Rais Samia na amebainisha kuwa baada ya mazungumzo hayo taasisi hiyo ipo tayari kuendeleza miradi hiyo kwa kushirikiana na Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Kwa upande wake, Mhe. Rais Samia ameishukuru taasisi hiyo kwa mchango wake katika masuala ya afya ya wanawake hapa nchini na amemhakikishia kuwa Serikali ya Tanzania ipo tayari kushirikiana nayo ili kukabiliana na changamoto zinawakabili wanawake na wasichana katika masuala ya afya.

Mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima na Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Aifello Sichwale ambao baadaye wamefanya mazungumzo na Bi. Senait Fisseha kwa lengo la kujipanga namna taasisi hiyo itakavyofanya kazi na Serikali.

 CHANZO: IKULU 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.