Star Tv

Chama cha ACT Wazalendo kimewafahamisha wanachama wake, pamoja na umma wa Watanzania kuwa Mwenyekiti wake Maalim Sei Sharif Hamad na mkewe Bi Awena, wamethibitika kupata maambukizi ya Covid 19.

Kulingana na taarifa ya chama iliyotumwa kwenye mitandao yake ya kijamii, ACT Wazalendo imesema kuwa wasaidizi kadhaa wa Makamu huyo wa Rais wa Zanzibar pia wamepatikana na virusi vya corona baada ya kufanyiwa vipimo.

''Katika hali ya kuchukua tahadhari zaidi madaktari walimshauri Maalim Seif kuwa ni vyema awepo chini ya uangalizi maalum katika kipindi chote atakachokuwa anaendelea na matibabu'', imesema taarifa ya ACT iliyotumwa kwenye ukurasa rasmi wa Twitter wa chama.

Kulingana na taarifa hiyo Maalim Seif amepumzishwa katika Hospitali ya Mzazi Mmoja, Unguja, ambako anaendelea kuwa chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.