Star Tv

Mahakama ya India imemuondolea mashtaka askofu mmoja aliyeshtakiwa kwa kumbaka mtawa mmoja kati ya mwaka wa 2014 na 2016 katika kesi ambayo ilishtua jumuiya kongwe za Kikristo nchini humo.

Franco Mulakkal, mwenye umri wa miaka 54, alikamatwa kutoka jimbo la kusini la Kerala mwaka wa 2018 na alikuwa amekanusha madai hayo.

Kesi hiyo ilizua maandamano makubwa baada ya mtawa huyo kudai kuwa Kanisa Katoliki lilipuuza malalamishi yake.

Vatikani ilikuwa imemwondolea askofu kazi zake kwa muda.

Siku ya Ijumaa, mahakama ya mjini Kottayam ya Kerala ilimkuta hana hatia ya mashtaka. "Upande wa mashtaka ulishindwa kuthibitisha mashtaka yote dhidi ya mshtakiwa," alisema Jaji wa vikao vya ziada vya Kottayam (ASJ) G Gopakumar.

Mawakili wa mtawa huyo walisema watapinga uamuzi huo katika mahakama kuu.

Lakini timu ya wanasheria ya askofu huyo ilisema "imesambaratisha ushahidi wote" dhidi yake. "

Bw Mulakkal alikuwa askofu wa dayosisi ya Jalandhar katika jimbo la kaskazini la Punjab.

Mshitaki wake ni wa Wamisionari wa Yesu, huko Kerala ambalo ni sehemu ya dayosisi ya Jalandhar. A

Aidha Mtawa huyo alidai kuwa Askofu huyo alimbaka mara 13 na mashambulizi hayo yalitokea alipotembelea nyumba ya watawa alikokuwa akiishi katika jiji la Kottayam, Kerala.

#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.