Star Tv

Taliban imepiga marufuku matumizi ya fedha za kigeni nchini Afghanistan, hatua ambayo inaelezwa kwamba itaathiri zaidi uchumi wao ambao unaporomoka.

Taliban inafikia hatua hiyo mara baada ya hali ya kiuchumi bado haijatengamaa kutokana na kujiondoa kwa msaada wa kifedha wa kimataifa mara baada ya Taliban kuingia madarakani.

"Hali ya ya uchumi na matakwa ya taifa katika nchi yanahitaji raia wote wa Afghans kutumia fedha za Afghani katika biashara zao,"- Taliban ilisema.

Dola ya Marekani ilikuwa ikitumka zaidi katika masoko ya Afghanistan.

Dola pia zimekuwa zikitumika mara nyingi katika biashara za maeneo ya mpakani mwa Afghanistan kama Pakistan.

"Yeyote atakayekiuka sheria hii atakabiliwa na hatua za kisheria,"- taarifa Kutoka nchini humo zimeeleza.

Baada ya Taliban kudhibiti taifa hilo mwezi Agosti, mabilioni ya dola yaliyokuwa nje ya nchi yalitaifishwa na Marekani.

#ChanzoBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.