Star Tv

Shirika la Afya Duniani limesema limesikitishwa na madai ya unyanyasaji wa ngono unaofanywa na wafanyakazi wake nchini DRC wakati wa mlipuko wa Ebola.

Madai hayo ambayo yalikuja, mwaka mmoja baada ya uchunguzi uliofanywa na shirika la habari za masuala ya kibinadamu na taasisi ya Thomson Reuters.

Wanawake wa eneo hilo walidai kunyweshwa pombe, kuviziwa na kulazimishwa kufanya ngono na wawili walipata ujauzito.

Mkurugenzi wa WHO barani Afrika, Matshidiso Moeti ameomba radhi kwa wanawake na wasichana waliopata masaibu hayo kwa mwaka 2018 na 2020 kwasababu hatua kali zitachukuliwa kwa wafanyakazi hao na watumishi wengine wa afya.

Wachunguzi huru wanasema kuwa mfumo umeshindwa na uzembe wa mtu mmoja katika ripoti yao.

Katibu mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus alisema ripoti hiyo inafadhaisha kuisoma.

Aliomba radhi na kuongeza kuwa hataacha kuahidi kuwasaidia waathirika kwa ulinzi na kupata haki yao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.