Star Tv

Kiongozi wa Algeria ametangaza siku tatu za maombolezo kuanzia leo hii, kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa taifa hilo, Abdelaziz Bouteflika.

Rais huyo wa zamani wa Algeria, Abdelaziz Bouteflika, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 84 baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Bouteflika ambaye utawala wake wa miaka 20, unatajwa kugubikwa na rushwa na aliondoshwa madarakani kwa maandamano makubwa baada ya kutaka kugombea madaraka kwa muhula mpya.

Bouteflika aliyefikwa na maradhi ya kiharusi mwaka 2013, alifariki dunia Ijumaa, akiwa na umri wa miaka 84.

Katika siku zake za mwisho za urais wake alikuwa akionekana kwa nadra sana.

Rais huyo zamani hajaonekana kabisa hadharani tangu, Rais Abdelmadjid Tebboune achukue hatamu ya uongozi wa Algeria.

Ofisi ya rais huyo wa sasa imesema katika maombolezo hayo ya siku 3 bendera zitapepea kwa nusu mlingoti.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.