Star Tv

Rafiki wa zamani wa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema anataka kuunda serikali ya muungano na upinzani nchini humo, hiyo ikiwa ni hatua kubwa katika kuufikisha mwisho utawala wa muda mrefu wa waziri huyo mkuu.

Tangazo hilo la Naftali Bennett, ambaye ni kiongozi wa chama kidogo cha Yamina, limetoa nafasi ya msururu wa hatua ambazo huenda zikamsukuma Netanyahu na chake cha Likud katika upinzani wiki ijayo. "Serikali itafanikiwa iwapo tu tutashirikiana kama kikundi. Sio mimi bali sisi. Tutarudisha neno "sisi" ambalo ndilo lililokuwa silaha ya siri ya Israel tangu siku ya kwanza. Vyama vyote vinaalikwa kuungana na serikali."Huku Bennett na washirika wake wapya wakiongozwa na kiongozi wa upinzani Yair Lapid wakiwa bado wana vigingi vingi mbele yao, pande hizo zinaonekana kuwa zimedhamiria kupata makubaliano. Makubaliano hayo yataufikisha mwisho mkwamo ambao umeipelekea nchi hiyo kushuhudia chaguzi nne katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.

CHANZO: IDHAA YA KISWAHILI (DW).

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.