Star Tv

Rais Mteule nchini Marekani kupitia Chama cha Demokrats amemteua Anthony Blinken kuwa Waziri wa mambo ya nje.

Duru za kisiasa nchini Marekani zimeripoti kuwa rais huyo mteule wa Marekani Joe Biden amemteua Anthony Blinken kuwa Waziri wa mambo ya nje, atakapochukua kiti cha urais rasmi.

Bw. Blinken ana uhusiano wa karibu na Bw Biden kwa takribani miaka 20, ambaye anaelezwa kuwa na uzoefu wa masuala ya kigeni.

Anafahamika kama mtu anayeunga mkono ushirika dhabiti na mataifa mengi, akisema mapema mwaka huu kwamba matatizo kama vile mabadiliko ya hali ya hewa, janga la corona na utengenezaji wa silaha hatari hayawezi kutatuliwa na Marekani peke yake.

Wakati mmoja aliwahi kuwa Naibu waziri wa mambo ya nje chini ya utawala wa rais wa zamani Barack Obama ambapo alisaidia kuboresha masuala ya ushirikiano na mataifa yaMashariki ya kati.

Bw Bilken, mwenye umri wa miaka 58, alisomea Ufaransa, na baadaye katika Chuo Kikuu cha Harvard University na Cho Kikuu cha Sheria cha Colombia.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.