Star Tv

Serikali ya Libya yadai kuuteka mji muhimu kutoka kwa hasimu wake Khalifa Haftar.

Vikosi vilivyo na mafungamano na serikali ya Libya inayotambulika kimataifa vimesema vimechukua udhibiti wa mji muhimu kutoka kwa mahasimu wao hii leo.

Haya yanatokea siku moja tu baada ya vikosi hivyo kuchukua udhibiti wa mji mkuu Tripoli.

Katika wiki za hivi majuzi vikosi hivyo vimepiga hatua kubwa katika kuyanyakua maeneo yaliyokuwa yanadhibitiwa na mbabe wa kivita Khalifa Haftar.

Msemaji wa serikali ya Waziri Mkuu Fayez el-Sarraj, Mohammed Gnounou amesema leo kuwa vikosi vya serikali vimeudhibiti kikamilifu mji wa Tarhouna, ulioko kilomita 90 kusini mashariki mwa Tripoli.

Msemaji wa jeshi la serikali hiyo inayotambulika kimataifa amesema vikosi vya serikali vimeingia katika mji wa Tarhouna bila mapigano baada ya vikosi vya Haftar kuondoka katika mji huo na kuelekea jangwani.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.