Serikali ya Libya yadai kuuteka mji muhimu kutoka kwa hasimu wake Khalifa Haftar.
Vikosi vilivyo na mafungamano na serikali ya Libya inayotambulika kimataifa vimesema vimechukua udhibiti wa mji muhimu kutoka kwa mahasimu wao hii leo.
Haya yanatokea siku moja tu baada ya vikosi hivyo kuchukua udhibiti wa mji mkuu Tripoli.
Katika wiki za hivi majuzi vikosi hivyo vimepiga hatua kubwa katika kuyanyakua maeneo yaliyokuwa yanadhibitiwa na mbabe wa kivita Khalifa Haftar.
Msemaji wa serikali ya Waziri Mkuu Fayez el-Sarraj, Mohammed Gnounou amesema leo kuwa vikosi vya serikali vimeudhibiti kikamilifu mji wa Tarhouna, ulioko kilomita 90 kusini mashariki mwa Tripoli.
Msemaji wa jeshi la serikali hiyo inayotambulika kimataifa amesema vikosi vya serikali vimeingia katika mji wa Tarhouna bila mapigano baada ya vikosi vya Haftar kuondoka katika mji huo na kuelekea jangwani.