Star Tv

Kirusi cha corona chazidi kusambaa duniani kwa kutia mguu Magharibi mwa Afrika ambapo mtu wa kwanza aliye na kirusi cha corona katika eneo la chini ya jangwa la Sahara Magharibi mwa Afrika amegunduliwa nchini Nigeria.

Waziri wa Afya wa Nigeria Osagie Ehanire ameeleza katika taarifa aliyotoa kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Twitter mapema leo kwamba, mtu huyo ni raia wa Italia anayefanya kazi nchini humo, ambaye alirejea Nigeria mapema wiki hii akitokea mjini Milan, Italia.

Amesema hali ya mtu huyo si mbaya na tayari amelazwa katika hospitali ya magonjwa ya kuambukiza ya Yaba mjini Lagos.

Kabla ya Nigeria, kulikuwa kumeripotiwa kesi mbili tu za maambukizi ya kirusi cha corona barani Afrika, moja ikiwa ni katika ya nchi ya Misri na nyingine nchini Algeria.

Wakati huohuo Lithuania nayo pia imemgundua mtu mwenye kirusi cha corona nchini humo.

Maafisa wa afya wa Ireland ya Kaskazini nao pia wametangaza kugunduliwa mtu aliyekumbwa na kirusi cha corona katika eneo hilo na kuifanya idadi ya watu walioambukizwa kirusi hicho nchini Uingereza kufikia 16.

Mbali na China, ambayo ni kitovu cha maambukizi ya kirusi cha corona, nchi za Ulaya Magharibi zina idadi kubwa zaidi ya watu waliokumbwa na kirusi hicho.

Baada ya watu waliofariki kwa kirusi cha corona nchini Italia kuongezeka na kufikia 17, Ufaransa imetangaza kuwa idadi ya watu waliokumbwa na kirusi hicho nchini humo imefikia 40 wakati idadi hiyo nchini Ujerumani ni 38.

                                             Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.