Star Tv

Senegal imemzawadia kila mchezaji wa timu ya taifa ya kandanda zawadi ya pesa taslimu na mashamba kufuatia ushindi wao katika Kombe la Mataifa ya Afrika.

Kila mchezaji wa timu alipokea zaidi ya $87,000 (£64,000) na kiwanja katika mji mkuu, Dakar, na katika mji jirani wa Diamniadio wakati wa sherehe iliyofanyika ikulu ya rais.

Rais Macky Sall pia aliteua timu hiyo katika Tuzo ya heshima kutoka kwa Rais ambayo ni maarufu nchini Senegal, huku mashabiki wakishangilia nje ya lango.

Rais hapo awali aliishukuru timu hiyo kwa kufika “kilele cha dimba hilo la Afrika” na kuleta ”fahari na heshima ambayo inaashiria watu wa kipekee. ”

Senegal iliishinda Misri kwa mikwaju ya penalti 4-2, na kuwa mabingwa wa michuano hiyo kwa mara ya kwanza katika historia yao.

#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.