Star Tv

Umoja wa Afrika umelaani wimbi la mapinduzi ya hivi karibuni ambalo limeshuhudia idadi kubwa ambayo haijawahi kushuhudiwa ya nchi wanachama zikisimamishwa kutoka umoja huo.

Hayo yamesemwa na mkuu wa baraza la amani na usalama wa Umoja huo Bankole Adeoye wakati kikao cha kila mwaka cha Umoja huo kikikaribia kumalizika.

Adeoye amewaambia wanahabari kwamba kila kiongozi wa Afrika katika baraza hilo amelaani wimbi hilo la mabadiliko ya serikali kinyume na katiba.

Mataifa manne wanachama yalisimamishwa uanchama wao katika Umoja huo tangu katikati ya mwaka 2021 kwasababu ya mabadiliko ya serikali kinyume na katiba.

Mapinduzi ya hivi karibuni zaidi yalitokea nchini Burkina Faso, ambapo wanajeshi walimuondoa madarakani rais Roch Marc Christian Kabore mwezi uliopita.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.