Star Tv

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi amesema hali sio nzuri lakini ipo katika udhibiti baada ya kuripuka kwa volcano katika eneo Goma huko mashariki mwa taifa hilo.

Akizungumza baada ya serikali yake kutangaza kwa makosa kutokea mlipuko mwingine wa volkano, ikiwa ni takribani juma moja baada ya mlipuko wa Mlima Nyiragongo.

Rais Tshisekedi ameonya kwa kusema kwa hali ilivyo mripuko unaweza kutokea kokote katika jiji la Goma kwa kuwataka wakazi wa mji huo kutoharakisha kurejea katika makazi yao.

Taarifa yake hiyo anaitoa baada ya kuwepo kwa ripoti zinazosema zaidi ya wakimbizi 1,000 wameondoka katika kambi walizokuwa wanahifadhiwa huko Rwanda kurejea Goma.

Takribani wakazi 400,000 waliokolewa katika eneo la mashariki la Goma, baada ya wiki moja ya matetemeko ya ardhi, yalitokana na mripuko wa moja ya vokano hai barani Afrika.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.