Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma amekana mashitaka ya ufisadi yaliyokuwa yakimkabili mwanzoni mwa kesi yake katika mahakama ya Pietermaritzburg.
Kiongozi huyo ambaye wakati mmoja aliwahi kusherehekewa kwa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi anatarajiwa kukana mashitaka ya udanganyifu na ulaghai katika kesi ambayo ilianza na mkataba wa silaha miaka ya 1990.
Zuma alidai kuwa yeye ni “mwathiriwa wa hujuma za kisiasa na kwamba mahakama nchini humo zinashirikiana na mahasimu wake wa kisiasa”.
Bwana Zuma pia anakabiliwa na madai mapya ya ufisadi na huenda akafungwa jela kwa kukiuka amri ya mahakama katika kesi nyingine tofauti.
Baadhi ya mashujaa wa ukombozi wa Afrika Kusini wamemshtumu Zuma huku wakimlinganisha na ‘jambazi na kuonya itachukua muda mrefu kurekebisha uharibifu’ alioufanya dhidi ya taasisi changa za nchi hiyo.
Chanzo:BBCSwahili