Star Tv

Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma amekana mashitaka ya ufisadi yaliyokuwa yakimkabili mwanzoni mwa kesi yake katika mahakama ya Pietermaritzburg.

Kiongozi huyo ambaye wakati mmoja aliwahi kusherehekewa kwa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi anatarajiwa kukana mashitaka ya udanganyifu na ulaghai katika kesi ambayo ilianza na mkataba wa silaha miaka ya 1990.

Zuma alidai kuwa yeye ni “mwathiriwa wa hujuma za kisiasa na kwamba mahakama nchini humo zinashirikiana na mahasimu wake wa kisiasa”.

Bwana Zuma pia anakabiliwa na madai mapya ya ufisadi na huenda akafungwa jela kwa kukiuka amri ya mahakama katika kesi nyingine tofauti.

Baadhi ya mashujaa wa ukombozi wa Afrika Kusini wamemshtumu Zuma huku wakimlinganisha na ‘jambazi na kuonya itachukua muda mrefu kurekebisha uharibifu’ alioufanya dhidi ya taasisi changa za nchi hiyo.
Chanzo:BBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.