Star Tv

Idadi isiyofahamika ya mamba wadogo hawajulikani walipo baada ya kutoroka katika shamba wanapofugwa eneo la Cape Magharibi Afrika Kusini Jumatano, kulingana na vyombo vya habari vya eneo hilo.

Juhudi za kutafuta mamba hao kila mmoja akiwa na urefu wa zaidi ya mita moja zinaendelea.

Aidha, inashukiwa kwamba huenda wamepata njia inayowapeleka kwenye mto Breede ulio karibu.

"Ni hatari kiasi fulani kwa jamii kwasababu wamekuwa wakifungwa na wamezoea chakula cha kawaida, hawajitafutii chakula".

Msemaji wa serikali eneo hilo James-Brent Styan pia amenukuliwa na gazeti la Times Live akisema kuwa wanyama hao ni hatari kama wengine wowote wale wa aina hiyo ambao ni hatari kwa binadamu.

Takribani mamba 20 wamerejeshwa katika shamba wanapofugwa, kulingana na afisa wa eneo aliyenukuliwa na Tovuti ya Eye Witness News.

Chanzo: BBC Swahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.