Mpenzi wa mwanariadha wa Kenya Agnes Tirop, amefikishwa mahakamani kama mshukiwa wa mauaji ya mwanariadha wa Kenya Agnes Tirop.
Hakimu amesema atawaruhusu polisi kumzuia Ibrahim Rotich kwa siku 20, wakati ambao pia atafanyiwa uchunguzi wa kiakili kubaini ikiwa anaweza kufunguliwa mashtaka.
Bwana Rotich alikamatwa wiki iliyopita mjini Mombasa Pwani ya Kenya na polisi wamearifu kuwa alikuwa akijaribu kutoroka nchini.
Agnes Tirop alipatikana akiwa ameuawa kwa kuchomwa kisu nyumbani kwake magharibi mwa Kenya.