Star Tv

Watu 32 wamethibitishwa kufariki kwenye ajali ya gari nchini Uganda iliyotokea usiku wa kuamukia leo katika wilaya ya Kasese.

Vifo hivyo vimetokea baada ya magari matano kugongana katika kijiji cha Kihongo kilichopo kwenye barabara kuu ya Hima –Rugendabara wilayani Kasese magharibi mwa Uganda.

Miili ya marehemu 32 imepatikana na majeruhi watano wamepelekwa katika hospitali ya Kilembe.

Katika taarifa iliyotolewa na shirika la Msalaba mwekundu nchini humo, timu yao ikishirikiana na jeshi la UPDF na Polisi ikiongozwa na Meja Charles Nzei wameweza kuwaokoa majeruhi na kupata miili ya waliofariki.

Sababu ya ajali hiyo imetajwa kuwa ni ufinyu wa barabara inayotengenezwa na kulikuwa giza kubwa na hivyo kusababisha Malori mawili kugongana mjini Kasese na kuanguka.

Baada ya yaliangukakwa malori mawili ambayo tayari , gari lingine kutoka Budibugyo pia likaanguka kwenye katika eneo hilo hilo.

Kwa pamoja magari 5 yakaanguka kwanye ajali iliyosababaisha vifo vya watu 32 na watano kujeruhiwa vibaya majira ya saa tatu za usiku kwa mujibu wa msemaji wa Red Cross Irene Nakasita.

Kati ya magari hayo L ori dogo ya aina ya kenta lilikuwa limebeba jeneza na watu waliokuwa wakielekea kwenye mazishi wakitoka wilayani Budibugyo wakielekea Kata ya Maliba.

Kwa mujibu wa takwimu za jeshi la polisi nchini Uganda karibu ajali za barabarani 20,000 hutokea kila mwaka nchini Uganda na kusababisha takribani vifo vya watu 2,000.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.