Star Tv

Polisi mkoa wa Mwanza kwa kushirikiana na vyombo vingine vya kiusalama wamewakamata watu saba waliojifanya ni maofisa wa usalama.

Watu hao wamedakwa wakidaiwa kujifanya maofisa usalama wa nchini Tanzania .

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza amesema watu hao wanatuhumiwa kuwatapeli wananchi na watumishi wa serikali huku wakiwajengea hofu wakazi wa jiji la Mwanza kwa mbinu ya mazingira ya kupewa rushwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 7, 2020, kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro amesema matukio hayo yametokea kati ya Disemba 27, 2019 na Januari 2, 2020 maeneo ya Nyakato wilaya ya  Nyamagana Mkoani Mwanza.

Muliro amesema watuhumiwa hao walikuwa wakitumia Gari aina ya Toyota la kubeba wagonjwa yenye usajili wa namba T.751 BNL ambalo walisema ni sehemu ya msafara wa viongozi wakuu.

 "Walikamatwa na makachero na wakaendelea kujitambulisha kuwa wao ni maofisa usalama wa taifa toka ikulu lakini walipohojiwa kwa kina ilibainika ni matapeli" -Jumanne Muliro-Kamanda wa Polisi Mwanza .

Kamanda Muliro amewataja watuhumiwa hao saba  kwa majina na umri kuwa ni: Chalanga Chalanga (45) mkazi wa Pasiansi Mwanza na Arusha, Hamis Mwalimu (25), Philipo Petro (35) mkazi wa Misungwi, Elia Gunda (30) mkazi wa Kisesa, Hassan Juma (29) mkazi wa Mkolani, Selemani Karanga (25) ambaye alijifanya mlinzi wa Chalanga Chalanga na Michael Mazigemkazi mkazi wa Morogoro.

Aidha, kamanda Muliro  amesema watuhumiwa tayari  wamehojiwa na upelelezi ukikamilika watafikishwa Mahakamani.

                                                                                  Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.