Star Tv

Wananchi  katika   kjiji cha  Kisungamile  kata  ya  matai   wilayani  Kalambo  mkoani  Rukwa  wameiomba  serikali  kufanya   marekebisho  ya   miundombinu  ya  maji  ambayo  imeharibiwa  na mifugo  na  hivyo  kupelekea  kukosekana kwa  huduma hiyo muhimu    kwa zaidi  ya mwezi  mmoja  na  hivyo  kulazimika  kutumia  maji  ya  visima  ambayo ni  hatari  kwa  afya  zao.

Kijiji  cha  kisungamile  kina  zaidi   ya  wananchi  elfumoja  (1000)  na  kina patikana   katika  kata  ya  Matai , kijiji  hiki  kimekuwa  kikikabiliwa  na  changamoto   kubwa  ya  ukosefu  wa  huduma  ya  maji na  huku  wananchi wake  wakilazimika  kutumia  maji  ya  mto Chimilango  pamoja  na  maji  ya visima  ambayo  si salama  kwa  afya  zao na  hivyo  kulazimika  kuitisha  mkutano  wa hadhara  ili  kujua  hatima  ya  swala  hilo.

Diwani  wa  kata   hiyo  Vitus  Tenganamba  amesema  serikali  inampango  wa   kuanzisha  mradi  mpya  wa  maji   kwenye  maeneo   hayo   na  kuwataka  wananchi  kuendelea  kuwa  na subira  wakati  swala  lao  likiendelea  kufanyiwa  kazi. Mkuu wa  wilaya  hiyo Julieth  Binyura  amewataka  wananchi  kuacha  kulima  kwenye  vyanzo  vya  maji kwa  lengo  la  kuondokana na adha   kuziba  kwa  mabomba  hususani  wakati  wa  masika. Inaelezwa  kuwa   chanzo  cha  kukatika  kwa  maji  kila  wakati  kwenye  maeneo  hayo  ni  kutokana na  wananchi  kulima  kwenye vyanzo  vyamaji na   huku  maji  yanayotoka   yakiwa  ni  machafu  muda  wote.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.