Mwamko mdogo miongoni mwa wanariadha wa Tanzania umewafanya wanariadha wa kenya kutamba katika mashindano ya Ngorongoro marathon. Mashindano ya Ngorongoro marathon ya kilometa 21 yamewakutanisha washiriki zaidi ya Mia tano kutoka mataifa mbalimbali yakiwa na lengo la kutangaza Utalii.
Waziri wa maliasili na Utalii Hamis Kigwangala aliongoza mashindano hayo amewataka watanzani kushiriki kikaamilifu katika shughuli za uhifadhi.
Hii ni mara ya kumi na mbili kwa michuano hiyo kufanyika hivyo hamasa inahitajika zaidi kwa lengo la kupata vipaji vipya vya medani ya riadha huku mshindi wa kwanzwa kwa wanawake na wanaume akijinyakulia shilingi milioni moja na mshidi wa pili akipata shilingi laki tano na watatu akiondoka na shilingi laki tatu.