Star Tv

MKE wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mariam Mwinyi ameiasa jamii kujitahidi kuongeza ibada mbalimbali ndani ya mwezi Mtukufu wa Ramadhan na kutoa sadaka kwa wingi hasa kuwafikia watu wenye mahitaji maalumu wakiwemo wazee, watotoyatima, wenyeulemavu na masikini ili kupata radhi za Mwenyezi Mungu (S.W).

Mama Mariam aliyasema hayo kwa nyakati tofauti alipowatembelea wazee wa Welezo na Sebleni pamoja na watoto yatima waliopo Kijiji cha SOS na Mazizini ,Mkoa wa Mjini Magharibi ambako aliwasalimia, kuwafariji na kuwapa zawadi ya futari pamoja na mabegi ya shule watotoyatima.

Amesema ibada ya sadaka sio lazima kutolewa zaidi kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani, bali hata siku za kawaida kwani zinaogeza upendo na kuigusa jamii yenye uhitaji. “Kama kawaida desturi yetu mwezi wa Ramadhan huwa tunatembeleana, kujuliana hali, sio desturi pekee lakini pia ni maagizo kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, anatutaka waja wake kutoa sadaka kwa wingi na kufanya zaidi mambo mazuri ya kumridhisha Yeye kama kuwakumbuka wazee, wajane, watu wasiojiweza na masikini kuwapa sadaka ili nao watekeleza vizuri ibada hii ya mwezi mtukufu wa Ramandani” Alisema Mama Mariam. Miongoni mwa msaada waliopatiwa wazee na watoto hao ni pamoja na tende, vyakula vikiwemo mchele, unga wa ngano, sembe, mafuta ya kupikia, sukari pamoja na vyakula vya nafaka.

CHANZO: IKULU ZANZIBAR

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.