Makamu wa Rais wa Marekani Bi, Kamala Harris, amewasili nchini Tanzania na kupokelewa na Makamu wa Rais wa Tanzania Dk, Philipo Mpango.
Hii ikiwa ni mara yake ya kwanza kutembelea nchini hapa, ambaye ameambatana na mumewe kwa mualiko maalum kutoka kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu. Makamu wa Rais Kamala atakuwa na ziara ya Siku tatu.
Huku Marekani imekuwa ni mshirika mkubwa wa maendeleo na pia atakuwa na mazungumzo na Rais Dk; Samia Suluhu, lengo likiwa ni kuimarisha mahusiano baina ya pande mbili hali kadhalika mengine yanayotarajiwa kuongelewa ni pamoja na suala la maendeleo ya uchumi, mabadiliko ya Tabia nchi, usalama wa chakula pamoja na maendeleo ya demokrasia na mengineyo ambayo ni ajenda kuu katika ziara yake hii nchini Tanzania. Vile vile atapata nafasi ya kukutana na wasanii wa Tanzania katika na kuongelea juu ya kazi zao na ushirikiano baina ya mataifa haya. Ikiwa ni muunganiko wa ziara anazofanya Africa ambapo ameanzia ziara yake nchini Ghana, kisha atamalizia nchini Zambia.