Star Tv

Makamu wa Rais wa Marekani Bi, Kamala Harris, amewasili nchini Tanzania na kupokelewa na Makamu wa Rais wa Tanzania Dk, Philipo Mpango.

Hii ikiwa ni mara yake ya kwanza kutembelea nchini hapa, ambaye ameambatana na mumewe kwa mualiko maalum kutoka kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu. Makamu wa Rais Kamala atakuwa na ziara ya Siku tatu.

Huku Marekani imekuwa ni mshirika mkubwa wa maendeleo na pia atakuwa na mazungumzo na Rais Dk; Samia Suluhu, lengo likiwa ni kuimarisha mahusiano baina ya pande mbili hali kadhalika mengine yanayotarajiwa kuongelewa ni pamoja na suala la maendeleo ya uchumi, mabadiliko ya Tabia nchi, usalama wa chakula pamoja na maendeleo ya demokrasia na mengineyo ambayo ni ajenda kuu katika ziara yake hii nchini Tanzania. Vile vile atapata nafasi ya kukutana na wasanii wa Tanzania katika na kuongelea juu ya kazi zao na ushirikiano baina ya mataifa haya. Ikiwa ni muunganiko wa ziara anazofanya Africa ambapo ameanzia ziara yake nchini Ghana, kisha atamalizia nchini Zambia.

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.