Mpango wa idara ya afya wa kutoa elimu ya afya ya uzazi na matumizi ya uzazi wa mpango unatajwa kusaidia kupunguza mimba za utotoni na vifo vitokanavyo na utoaji wa mimba usio salama kwa makundi ya vijana katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya.
Mimba za utotoni na vifo vitokanavyo na utoaji wa mimba usio salama, ni moja ya changamoto inayatajwa kuwakabili vijana wengi wakike katika Halmashauri ya ya Jiji la Mbeya hayo yakibainishwa na mratibu wa afya ya uzazi wa mama na mtoto idara ya afya Jiji la Mbeya Akwina Mtweve; 'Amesema kutokana na elimu wanayoitoa mara kwa mara imesaidia kupunguza hali hiyo. Huku Shirika la Jhpiego kupitia mradi wake wa 'The challenge initiative TCI',kwa kushirikiana na serikali ndiyo wanatekeleza mpango huo wa kutoe elimu kwa makundi mbalimbali, akifafanua mratibu wa TCI mkoa wa Mbeya bwana, Waziri Njau. Huku lengo la uongozi wa Jiji la Mbeya ni kuona mimba za utotoni na vifo vitokanavyo na utoaji wa mimba usio salama vinakomeshwa.