Star Tv

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesogeza mbele hukumu ya kesi ya kutoa taarifa ya uongo kupitia mtandao wa Facebook, inayomkabili Bob Chacha Wangwe, November 8,2017.

Bob ambaye ni Mwanaharakati ni mtoto wa marehemu Chacha Wangwe, aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Tarime, mkoani Mara na Makamu Mwenyekiti wa Chadema-Bara.

Hukumu hiyo ilitarajiwa kusomwa leo na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ambapo amesema ameshamaliza kuiandaa hukumu hiyo lakini anaona ni vyema akaisoma tarehe ijayo.

“Hukumu nimeshamaliza kuiandaa kila kitu, hivyo nitaisoma November 15,2017,”.

Katika kesi hiyo, upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi 6, upande wa utetezi ukiwa na shahidi mmoja ambaye ni mshtakiwa mwenyewe.

Awali katika ushahidi wake, Bob amedai kuwa yeye hakuandika maneno ya upotoshaji wala hajawahi kufanya hivyo.

“Mimi nilitoa maoni yangu kuhusu uchaguzi wa Zanzibar na kasoro zake za kidemokrasia kama Watanzania wengine na waangalizi wa uchaguzi huo walivyofanya,”.

Katika kesi hiyo namba 167, Chacha Wange anatuhumiwa kwa kosa la kuchapisha taarifa za kupotosha katika ukurasa wake wa mtandao wa Facebook.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.