Rais Magufuli leo May 30,2020 Mkoani Dodoma amewakabidhi Marais Wastaafu wa Tanzania kila mmoja Tausi 25 wanaopatikana Ikulu ya Chamwino.
Marais hao pamoja na Mama Maria Nyerere wamepewa tausi hao ili wakawatunze kwenye bustani zao.
Mama Maria Nyerere amekabidhiwa tausi hao kwa niaba ya Baba wa Taifa Mwl. Nyerere.
“Tausi hawa ambao kila Rais Mstaafu nimemkabidhi 25 wataanza kuondoka leo hii tumeshaandaa utaratibu kuwasafirisha kwenda Butiama, Msoga nk, ikitokea mmoja akafia njiani tutareplace (zimetolewa pia kilo 100 za chakula cha Tausi cha kuanzia kwa kila mmoja)”-JPM
Rais Magufuli amesema Tanzania haikuwahi kuwa na tausi, tausi hao waliltetwa na Baba wa Taifa na Mama Maria Nyerere anaifahamu zaidi historia yake.Mzee Mwinyi aliwakuta hakuwachinja kuwala nyama maana nyama yake tamu kuliko kuku,Pia rais Mkapa na Kikwete waliwatunza.