Star Tv

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli anasikitika kutangaza kifo cha Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Balozi Dkt.Augustine Mahiga (Mbunge) kilichotokea leo Alfajiri tarehe 01 Mei,2020. Jijini Dodoma.

Mhe.Balozi Mahiga ameugua akiwa nyumbani kwake Jijini Dodoma na amefikishwa hospitali akiwa ameshafariki dunia.

Rais Magufuli ametoa salamu zake za pole kwa familia ya Marehemu, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai, Wabunge, Wafanyakazi wa Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na wananchi wa Iringa, ambapo amesema anaungana nao katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

Aidha, amemuelezea Marehemu Balozi Mahiga kama mchapakazi, muadilifu, mzalendo na mwanadiplomasia mahiri aliyeiwakilisha na kuipigania Tanzania katika Nyanja za Kimataifa kwa miaka mingi.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.