Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Augustino Ramadhan amefariki Duni leo saa mbili asubuhi katika Hospitali ya Agha Khan iliyopo Dar es Salaam baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Marehemu Jaji Ramadhan aliwahi kutumikia nafasi mbalimbali na kupata vyeo vya juu katika serikali ya Tanzania ikiwemo kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Tanzania Bara na Visiwani mwaka 2002 hadi 2007, pia Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar katika kipindi hichohicho.
Pia alishakuwa Brigedia Jenerali ambapo aliwahi kulitumikia Jeshi, na hadi anafariki alikuwa ni Mchungaji wa Dayosisi ya Kanisa la Anglikana lililopo Mkunazini Zanzibar, na Jaji Mstaafu Ramdhani aliwahi kuwa Jaji Mkuu Zanzibar.