Star Tv

Mwenyekiti wa Ngome ya Wazee wa Chama cha ACT Wazalendo Wilson Mushumbusi ameiomba Serikali kuunda Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi itakayosimamia uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka huu kwa kuzingatia misingi ya haki na demokrasia.

 Taarifa na Rachel Dickson.

Hayo yamejiri wakati akihutubia mkutano wa kuchagua mwenyekiti wa ngome ya wazee wa chama cha ACT Wazalendo jijini Dar es salaamWilson Mushumbusi amesema tume huru itasaidia kuondoa ubaguzi wa wazee kwa misingi ya milengo ya vyama vya siasa.

Kwa upande wake Mwenyikiti wa Taasisi Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku amesema uchaguzi huo Ngome ya Wazee wa chama cha ACT Wazalendo utaleta mabadiliko katika kuwasimamia wazee hasa katika chama kwa usawa na haki.

Uchaguzi wa ngome ya wazee wa Chama cha ACT Wazalendo ni wa tatu ndani ya chama hiyo ukitanguliwa na ule wa wanawake na vijana huku ikiwa imebakia wa kumchagua kiongozi wa mkuu wa chama ambao unatarajia kufanyika hivi karibuni.

                  Mwisho.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.