Star Tv

Viongozi mkoani Tabora wameiomba serikali kuhakikisha inawakamata watu waliohusika katika tukio la mauaji ya Diwani wa Kata ya Usunga Alfed Masamalo wilayani Sikonge mkoani Tabora.

Taarifa na Sunday Kabaye

Viongozi hao wakiwemo wa dini wametoa ombi hilo kwa serikali kufuatia kutokea kwa matukio ya mauaji  mfululizo ikiwemo tukio la kukatwakatwa mapanga kwa Mhandisi wa maji katika wilaya ya Sikonge hadi umauti kumpata siku za hivi karibu.

Baada ya kupokea maombi kutoka kwa viongozi hao Mkuu wa mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri ambaye aliongoza mamia ya wakazi wa mkoa wa Tabora katika mazishi ya diwani huyo aliyeuwawa kwa kukatwa mapanga katika sehemu za mwili wake ameagiza vyombo vya usalama kuhakikisha wanafanya operesheni na kuwakamata wote wanaohusika na matukio ya mauaji yanayoendelea mkoani Tabora

Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora Kamishina Msaidizi wa Polisi Laurian Fabian amesema tayari jeshi hilo linawashikilia watu sita wanaotuhumiwa kuhusika na tukio la kifo cha diwani huyo.

Katika maeneo mbalimbali ya mkoani Tabora hivi karibuni kumekuwepo na mfululizo wa matukio ya watu kuuawa kikatili wakiwemo Wananchi na watumishi wa serikali jambo linaloanza kuleta hofu kwa wakazi wa mkoa wa Tabora.

                                  Mwisho.

 

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.