Star Tv

Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania TEC Padre Dokta Charles Kitima amesema kipindi cha kwaresima ni fursa ya kujitafakari na kumpa Mungu nafasi ya kwanza katika maisha pamoja na kutambua nafasi ya Mwenyezi Mungu kwa maisha ya kila siku kwa wakristo na wasio wakristo.

Taarifa na Piensia Rugarabamu

Padre Dokta Charles Kitima ametoa kauli hiyo wakati wakristo wakielekea katika mwezi wa toba ambapo amewataka waumini kote nchini kutambua nafasi ya muumba katika maisha yao pamoja na kubadilisha mahusiano yao mabaya na Mwenyezi Mungu.

Kwa upande wake Padre Hesco Msaga amesema kipindi cha kwaresma ni safari ya kiroho ambayo kila mkatoliki anatakiwa kutafakari na kujiandaa nafsi yake na kujiweka tayari katika kipindi hiki cha toba

Katika hatua nyingine Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dokta John Magufuli na mkewe mama Janeth Magufuli wameshiriki ibada ya jumatano ya majivu katika kanisa la mtakatifu petro jijini Dar es salaam.

                             Mwisho.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.